simplex

Deutsch-Tansanische Freundschaftsgesellschaft e.V.

Semina

Semina

Tangumwaka wa  2001 chama cha DETAF kinaandaa semina mara moja kwa mwaka, kuhusu mada mbalimbali zinazohusu Tanzania kwa yeyote anayependa kushiriki. Lengo la kongamano ni kuwapa watu fursa ya  kuifahamu vizuri zaidi nchi ya Tanzania,watu wake na utamaduni wao, hata kama hawatasafiri kwenda Tanzania.

Mada ya semina itakayofanyika wa mwaka huu itakuwa ni dini. Ukipenda kushiriki katika  semina hiyo  kama msemaji wasiliana nasi. Semina itafanyika tena mwanzoni mwa mwezi Mei katika mji wa Königswinter karibu na Bonn.

Mada zilizotangulia:

Maendeleoya  kiuchumi Tanzania tangu Ujamaa – 2007
Sanaa na fasihi Tanzania – 2006
Semina kuhusu vita vya majimaji – 2005
Tanzania ikolojia na utalii – 2004
Wanawake Tanzania – 2003                
Ugavi wa matibabu – 2002
Elimu – njia ya kuondoa umaskini – 2001

Ripoti kuhusu semina zetu zinapatikana katika archive (nyaraka) zetu na picha katika gallery.